Monday, October 1, 2018


MAJIRA MPYA YA KANISA
                                                                                                    
   
                                                                      







Na:








Mtume na Nabii Eliya Ad2 MUNGU wa Mjeshi

 MAJIRA MPYA YA KANISA

UFUNGUO
     Siku ya 28 Adari 2011 ambayo, kidunia inajulikana kama Februari 28 2012, kanisa, yaani The Pool of Siloam Church, liliendesha ibada ya kutoka miaka elfu sita (6000) na kuingia miaka elfu moja (1000) ya kutawala na Kristo YESU, kama ilivyounuliwa katika Ufunuo wa Yohana 20:4-5.
Kabla ya tarehe hiyo, katika mwaka wa 2008, kanisa lilitangaza Majira na Nyakati za kiungu ambazo zilikuwa na siku saba (7) za uumbaji na miezi kumi na mbili ya kiungu, kama inavyosomeka katika kitabu cha Mwanzo moja yote na Esta 3:7.
Kuanzia kipindi hicho kanisa, The Pool of Siloam Church,lilichapisha kitabu ambacho kinaonyesha  kuwa mwanzo wa mwaka siyo Januari, wala mwisho wa mwaka siyo Desemba, bali ni Adari, ambayo dunia na ulimwengu waliita Februari. Aidha, The Pool of Siloam Church tumekuwa, kuanzia mwaka 2008, hatufanyi ibada ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Bwana YESU tarehe 25 Desemba kama Dini na Madhehebu wanavyofanya, bali tarehe 28 Adari, kwa kuwa hiyo ndiyo siku sahihi ambayo YESU alizaliwa.
Pia, kanisa, tumekuwa tukifanya ibada ya Pasaka ya kweli mwezi wa Abibu, ambao ni mwezi wa kwanza, kila tarehe 14-21, kama inavyofunuliwa katika kitabu cha Kutoka 12:18; kama agizo la MUNGU katika kitabu hiki juu ya pasaka lilivyo la milele. Hivi sasa Pasaka ya kweli, ambayo maana yake ni kutoka kwenye utumwa wa kila aina, ni kila mwezi lango la 14-21.
Katika ibada zote za kila siku ambazo kanisa linafanyakuanzia saa kumi na moja alfajiri, tumekuwa tukiungana na wingu au unabii wa siku ya kwanza hadi ya saba, kulingana na kile alichokisema MUNGU siku hiyo, na wingu au unabii wa mwezi, kulingana na kilichofunuliwa katika mwezi wa kiungu husika, kama utakavyosoma kule mbele.

Hata hivyo kwa kipindi chote hicho, hatukuwa tumeachana na majira ya miaka elfu sita (6000) iliyopita kwa kuwa majira mpya ya kuanza siku ya kwanza, wiki ya kwanza, mwezi wa kwanza na mwaka wa kwanza ilikuwa haijarejea. 
Hivyo kwa ajili ya uelewa wa umma wote, Kanisa linapenda kufafanua kuwa MUNGU aliposema, katika kitabu cha Mwanzo 1:1-3 iwe nuru na ikawa nuru”; uumbaji ulipata siku ya kwanza, wiki ya kwanza, mwezi wa kwanza namwaka wa kwanza kwa mara ya kwanza.
Katika kitabu cha Mwanzo 7:23, tunasoma pia kwamba, baada ya miaka 2000 kupita, gharika ilitokea kila kitu chenye uhai kikafutwa isipokuwa Nuhu na familia yake. Baada ya Gharika, pale tena tulipata siku ya kwanza, wiki ya kwanza mwezi wa kwanza, na mwaka wa kwanza kwa mara ya pili ndani ya uumbaji wote.
YESU Kristo alipozaliwa katika Mathayo 2:1 na  Luka 2:1baada ya miaka mingine elfu mbili (2000), ndipo majira ilibadilika tena na kuanza siku ya kwanza, wiki ya kwanza,mwezi wa kwanza na mwaka wa kwanza kwa mara ya tatuna ndiyo maana tunasema hivi sasa, ni mwezi Adari 2011 au kidunia Februari 2012; ingawa tangu uumbaji imekwishapita miaka elfu sita (6000).
28 Adari 2011 (28 Februari 2012)   

Kanisa, The Pool of Siloam Church, linapenda kufahamisha jamii yote kuwa, ilipofika siku ya kwanza Abibu 2012 kidunia wanaita siku ya kwanza Machi 2012, tulianzamajira na nyakati mpya za Kiungu ambazo zilikuwepo hata kabla ya kuumbwa kwa kerubi, kama inavyofunuliwa katika Ezekiel 28:15. Mwezi sasa una siku ishirini na nane (28) peke yake. Maana siku ya 29, 30, na 31 iliongezwa kwa ufahamu wa kidunia ili kupingana na majira ya kiungu. Wasomaji wa tovuti ya www.dates in history.com wanafahamu kuwa siku hizi tatu (3) za ziada katika kila mwezi ziliongezwa na Papa Gregori wa kumi na tatuambaye 24 Adari 1582 (24 Februari 1582) alitangaza kalenda ambayo wote tunaoishi hivi sasa tumekuta ikitumika shuleni na maofisini.
Ili uthibitishe kuwa kwenye uumbaji wa majira ya MUNGU hakuna hizo siku 29,30 na 31 kwa kila mwezi, mzunguko wa siku za akina mama ni siku 28 tu wakati hata mtoto tumboni mwa mama tangu ile siku anapotungwa mimba hadi siku anayozaliwa, wauguzi wanahesabu wiki za mtoto na siyo miezi ili wasije wakachanganywa na kalenda ya Gregori yenye siku zaidi ya uumbaji wa MUNGU! 
Hivyo badala ya mwaka kuwa na siku 365, sasa una siku 336 kama kitabu cha Isaya 33:6 kinavyosema kuwa nyakati za kanisa zitakuwa imara, wokovu tele, hekima na maarifa.

Kwa mantiki hiyo, kwa mara ya nne, ndani ya uumbaji, tunapata tena siku ya kwanza, wiki ya kwanza, mwezi wa kwanza na mwaka wa kwanza (1, 1, 1, 1).
Tofauti ya Majira Mpya ya Iliyopita

Jambo kubwa linalotofautisha miaka 6000 iliyopita na hii miaka 1000 tuliyoingia ndani yake ni la siku ya saba kama linavyosomeka kaika kitabu cha Mwanzo 2:1-4. Katika mstari wa kwanza, kitabu kinasema “mbingu na nchi zikamalizika na jeshi lake lote”. Mstari unaofuata kitabu kinasema kuwa “MUNGU alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe. Mistari miwili inayofuata ina maneno mawili makuu, kuwa MUNGU aliitakasa hiyo siku ya saba na pia aliibariki.
Tafsiri ya kifungu hiki cha kitabu cha neno la MUNGU  tunaipata vizuri katika 2Petro 3:8 na Zaburi 90:4ambapo neno linasema “Miaka elfu machoni pako ni kama siku ya jana ikiisha kupita, na kama kesha la usiku”.
Hivyo, kwa kuwa kwa MUNGU, miaka 1000 ni sawa na siku moja, ina maana miaka hiyo yote 6000 iliyopita ni sawa na siku sita (6) peke yake. Kumbuka MUNGU aliumba kila kitu kwa siku 6 alipofika siku ya saba (7) akastarehe. Tunapoingia katika Miaka 1000 ya Kanisa kutawala na kumiliki na YESU, sawa na Ufunuo wa Yohana 20:4-5; ina maana tumeingia siku ya saba ya kubarikiwa, kustareheshwa baada ya kutakaswa kwa njia ya kuvunja misingi mibaya yote ndani ya watu na maeneo wanamoishi.

Kwa hiyo kipindi kile cha kwanza namba hii 1,1,1,1 ilipotokea mara tatu, shetani ndiye aliyekuwa bado anatawala wakati hivi sasa namba hii,1,1,1,1 inatokea na kutangazwa kwa mara ya nne, shetani,  nyoka wa zamani,akiwa hatawali tena ndani ya uumbaji. Ndiyo maana 28 Adari 2011(Feb.28 2012), YESU anazaliwa si tena katika hori la kulia ng’ombe, bali katika Jumba la Kifalme (yaani ndani ya hekalu la BWANA lililotakaswa) kama ilivyoandikwa katika I Korintho 3:16.

Siku hii ya saba, ambayo ni sawa na miaka 1000 ya Kanisa kutawala na YESU Kristo, ni sawa na kusema kuwa Kanisa limeingia kwenye majira na hatima mpya. Katika kitabu cha Muhubiri 9:11-12 na Waefeso 6:12-13 tunakutana na dhana ya majira inayoitwa wakati mbayana siku ya Uovu. Huko nyuma kwa sababu ya kubadilisha majra na nyakati za MUNGU, Kanisa lilijikuta linapita kwenye wakati mbaya wa kudharauliwa na kuchekwa. Kila kitu kibaya (kwa mfano magonjwa) kilihifadhiwa na huu wakati mbaya. Kwa hii majira mpya na hatima mpya ya kanisa, magonjwa, kudharauliwa na maonezi kinyume na kanisa havitakuwepo tena milele katika jina la YESU. Uovu wote na matendo yote kinyume na MUNGU, havitakuwepo tena. Majira hii mpya inafanyakazi na wana wa MUNGU kama inavyofafanuliwa hapo chini:

Kuna faida gani kutembea katika Majira na nyakati za kanisa?
Huko nyuma wengi hatukuwa tunajua kwamba Monday ni Moon-day yaani siku ya kuabudu mwezi. Hatukujua pia kwamba Sunday ni Sun-day, yaani siku ya kuabudu jua!Kwa hiyo wiki nzima hata useme nimeokoka kwa kuwa uko Monday (Jumatatu) hadi Sunday (Jumapili) kumbe ulikuwa umezingirwa na mungu mwezi na mungu jua! Ndiyo maana dini na madhehebu wameishia hapo walipoishia na miaka yao elfu sita (6000).
Aidha, huko nyuma wengi kama si wote, hatukujua kuwa kumbe Januari siyo mwezi wa kwanza wa mwaka na Desemba siyo mwezi wa kumi na mbili katika mwaka. Walioanzisha hiyo miezi ambayo ni miungu ya magharibi ndiyo wenye kujua siri ambayo bila shaka walipeana na waishio mashariki ya mbali.
Ni ajabu hadi leo, kwamba ukienda mashariki ya mbali,kwa mfano China, mwisho wa mwaka siyo Desemba bali ni Februari (ingawa walikuwa hawaelezi chanzo chake)! Ni ajabu pia benki nyingi hawafungi mahesabu yao Desemba bali Februari kwa kuwa wanajua huo ndio mwezi wa Adari aliozaliwa YESU Kristo, ambao ndio mwisho wa mwaka halisi!
Hata walioleta dini na madhehebu yanayojulikana,  nao wakadanganyika bila kujua kwamba, majira halisi ya kiungu (ambayo ndiyo majira ya kanisa yalichezewa).

Tunamshukuru MUNGU hata hivyo kwamba, kupitia kuhani afundishaye (II Nyakati 15:3) kanisa na taifa pia, tumetambua majira halisi ya MUNGU.

Katika kitabu cha Kutoka 14:19-24 tunaona kuwa wana wa Israeli walipokuwa wakitembea kutoka Misri kwenda Kaanani, waliongozwa na MUNGU kwa kutumia ishara mbili:
= Nuruni (wakati huo wakiita usiku) kulikuwepo na nguzo ya moto;  na 
= Mchana kulikuwepo na wingu la moto.
Ishara hizo mbili zilionyesha kuwa MUNGU alikuwa na wana wa Israeli katika kila sekunde, dakika, masaa na siku zote. Ndivyo ilivyo kuanzia sasa kwa wana wa MUNGU wote. Hawatatembelea tena Jumatatu hadi Jumapili wala Januari hadi Desemba, bali watakuwa na nguzo ya moto au wingu la moto kila siku likiwafunika, kupitia siku ya kwanza hadi ya saba na kupitia mwezi wa Abibu hadi wa Adari, kama ilivyofafanuliwa hapo chini:
SIKU SABA ZA UUMBAJI

Siku ya Kwanza- Nuru (Mwa. 1:1-5)
Jumatatu hadi Jumapili alikuwa anaruhusu giza, ukiwa na utupu, hata kama ungekuwa mwombaji sana. Hii ilikuwa inatokana na mtawala na mmiliki wa majira ya miaka 6000 iliyopita aliyekuwa ni uzao wa nyoka. Maneno mazuri tuliyowahi kunenewa na wachungaji wakiyasoma kutoka kwenye kitabu yalikuwa hayatimii hata kidogo. Maana kinachobeba kila kitu cha mtu, mwanadamu (hata mwana wa MUNGU) ni majira aliyomo.

Sasa yale aliyotamka MUNGU kuwa iwe nuru, na ikawa nuru yametimia. Hakuna tena atakayeingiza giza la uchawi, ushirikina, unajimu, ulozi, dua mbaya, umaskini, magonjwa au ufukara. Ni nuru ambayo sasa inaangaza katika maisha ya wana wa MUNGU na hasa ukizingatia kwamba wasimamizi wa giza sasa wametiwa wazimu na MUNGU mwenyewe (Isaya 44:25).
Siku ya Pili – Kuona (Mwa. 1:6-8)
Huko nyuma tukiwa katika giza na upofu unaotokana na siku ya kuabudu mwezi (Monday) hadi siku ya kuabudu jua(Sunday) tulikuwa hatuoni fursa mbali mbali (ingawa wageni wao wakija walikuwa wanaziona).
Katika kipindi hiki tumepewa macho saba ya MUNGU, kama YESU mwenyewe alivyo (Ufunuo wa Yohana 5:6).Hivyo uovu, tunauona na kuufuta kwa mamlaka ya jina la YESU. Baraka zetu nazo sasa tunaziona, na ndiyo maana katika Isaya 62:3-4 imeandikwa kwamba tumevikwa kilemba cha uzuri na kwamba kanisa na taifa teule hatutaitwa tena walioachwa wala wenye ukiwa.
Siku ya Tatu – Thamani & Faida (Mwa 1:9-13)

Huko nyuma kila tulichokuwa tunafanya, hasa kanisa, kilionekana kuwa ni hasara tupu. Miradi, makampuni ya wana wa MUNGU na mashamba yalionekana kudumaa kwa kuwa njia zote za faida zilikuwa za mwilini (zilishikiliwa na nguvu za giza). Neno la MUNGU halikuonekana kuwa la faida duniani.

Hivi sasa, Mith.3:13-16 imetimia kuwa, yule mwenye hekima na ufahamu wa kiungu ndiye atakuwa na utajiri na heshima mkono wake wa kushoto wakati ana maisha marefu mkono wake wa kulia.  Hakuna tena tumaini kwa upande wa uchawi na uganga. Biashara ya kuwafanya wengine kuwa misukule imeishia hapo kama Isaya 65:16inavyothibitisha. Kila atakachofanya mwana wa MUNGU, hivi sasa kina faida maana Joshua 1:5 inasema kwambahakuna anayeweza tena kusimama mbele ya mwenye haki.
Siku ya Nne–Unabii wa Kanisa (Mwa 1:14-19)

Katika Ufunuo wa Yohana 11:6 imeandikwa kuwa huu ni wakati wa unabii wa wana wa MUNGU, hata wakibadili maji kuwa damu ya YESU inawezekana. Kwa sababu ya mapinduzi yaliyoleta majira ya dunia na ulimwengu, jua na mwezi ambao waliagizwa kuwa watawala wa mchana na nuruni (usiku) chini ya kanisa waligeuzwa na kutawala juu ya kanisa! Matokeo yake dunia ikawa inasema kuwa siku inaanzia saa sita nuruni (usiku) na siyo saa moja asubuhi! Kitendo hiki, kimesababisha, kwa muda wa miaka 6000 iliyopita kusiwepo na mchana. Ina maana kuwa kila siku ilikuwa ni usiku tu! Hakujacha hata siku moja!
Hiki ndicho kilikuwa kinasababisha unabii wa kanisa usitimie, lakini sasa katika miaka hii 1000 ya kanisa kutawala na YESU, unabii wa kanisa kama unavyoandikwa kuanzia kitabu cha Mwanzo hadi Ufunuo wa Yohana, unatimia kila siku kwa kila mwana wa MUNGU, katika jina la YESU.

Siku ya Tano – Mambo Makuu (Mwa. 1:20-23)
Katika majira ya miaka 6000 iliyopita, kanisa lilitawaliwa na unyonge wa kila aina kiutendaji, achilia mbali muonekano wake katika jamii, ingawa katika kitabu cha Waefeso 3:10 imeandikwa wazi kuwa ni kwa njia ya kanisa tu, falme na mamlaka, katika ulimwengu wa roho za shetani, zinaweza kutambua hekima ya MUNGU iliyo ya namna nyingi.
Katika kipindi cha majira na hatma mpya hii ya kanisa, ni lazima sasa ahadi zote za MUNGU, kuhusu kanisa, kama ile ya Efeso 1:22-23 ya kuweka uumbaji wote chini ya miggu ya YESU na kanisa, itimie. Hii ndiyo maana ya kufanya makuu sana kipindi hiki.
Siku ya Sita – Kumiliki na kutawala (Mwa. 1:24-31)

Katika kipindi cha utawala wa uzao wa nyoka, kanisa walipitia utumwa wa kila aina, ikiwemo umaskini na ufukara, ingawa kitabu kinasema kuwa fedha na dhahabu ni mali ya MUNGU (Hagai 2:8-9). Pamoja na MUNGU kumkabidhi Adamu bustani ya Edeni, baada ya kuanguka, alinyang’anywa kila kitu na nyoka na uzao wake. Kwa kuwa Adamu na Hawa, wanawakilisha uumbaji wa kanisa, ina maana aliyenguka siyo Adamu bali lilikuwa ni Kanisa.
Katika kipindi hiki cha miaka 1000 ya kutawala na Kristo, si tu kanisa limerejea kuwa kama kwenye Bustani ya Edeni, bali kuwa kama kipindi ambacho MUNGU alikuwa hata hajamuumba kerubi (Ezekiel 28:15(a)).



Siku ya Saba–Kustareheshwa Pande zote (Mwa 2:1-4)

Kama ilivyokwisha elezwa kule nyuma, kipindi chote hiki cha miaka 1000 ya kutawala na YESU, kinaitwa siku saba na ni cha kustareheshwa pande zote. Kustareheshwa pande zote kunatokana na miaka tisa (9) ambayo roho ya Eliya imepita na Matengenezo, Marejesho, Upatanisho na sasa kujenga kunaanza (Luka 1:16-18)

MIEZI KUMI NA MBILI YA KIUNGU
Mwezi wa Kwanza – Abibu/Nisani – Roho ya ukombozi (Kut.12:2, 23: 15)
Kutokana na Kifungo cha Januari hadi Desemba miezi ambayo tuliona kule nyuma kuwa ni miungu ya magharibi, hatukuwa na mwezi wa kwanza wala wa kumi na mbili wa kweli kila mwaka. Zile siku tatu ambazo, tuliona kwambaziliongezwa na kalenda ya Gregori, zilizalisha mwezi wa kumi na tatu wenye siku 27. Kuna mataifa  ndani ya uumbaji ambao hukiri mwaka kuwa na miezi kumi na tatu, wakati kitabu cha neno la MUNGU, katika   Esta 3:7kinakiri mwaka kuwa na miezi  kumi na mbili tu, kuanziaAbibu au Nisani (mwezi wa kwanza) hadi Adari (mwezi wa kumi na mbili).
Katika kitabu cha kutoka 12 wana wa Israeli, walikombolewa utumwani Misri katika mwezi kama huuwa Abivu au Nisani. Hivyo kanisa, kwa maana ya Wana wa MUNGU, tunatembea sasa na roho ya ukombozi kila siku; kwa ajili ya kuondoa kila aina ya vitanzi vilivyokuwa vimewahi kutufunga katika miaka hiyo 6000 ya utumwa wa Kanisa.

Mila, desturi, elimu ya dunia, dini na madhehebu, ni kati ya vitanzi vilivyokuwa vimefunga wengi shingoni, mikononi na miguuni (kiakili) bila wahusika kujijua. Ni kazi ya unabii au roho ya ukombozi inayobebwa na Abibu au Nisani kuwafungua wote wanaokubali kuingia hivi sasa katika ufalme wa MUNGU, yaani kanisa. Bila majira hii mpya, ilikuwa haiwezekani mtu au mwanadamu aliyefungwa kwa kuunganishwa na vizazi na vizazi kufunguliwa. Tunamshukuru MUNGU kwa ukombozi huu uliounganishwa na ufalme wa MUNGU kupitiaAbibu/Nisani, katika jina la YESU.

Dunia au uzao wa nyoka, walioleta Januari hadi Desemba, wao walikuwa wanatumia hii miezi ya kiungu, ingawa walikuwa hawawezi kukiri hadharani!  

Mwezi wa Pili – Zivu – Roho ya kujenga (Mwa.7:11,1Fal.6:1)
Katika kipindi hiki cha miaka ambayo nyoka na uzao wake walikuwa wanatawala, kanisa lilibomolewa sana. Kila kitu ambacho MUNGU alisema kiligeuzwa, kwa sababu ya majira na nyakati za kiungu kuharibiwa, pale katika Bustani ya Edeni.

Ndiyo maana hata agizo la Siloam (yaani aliyetumwakama inavyofunuliwa katika Yohana 9:7) ni roho ya kujenga kanisa. Hivyo kila ambaye afya, familia, kazi auhuduma yake ilikuwa imebomoka; sasa unabii wa zivu unamjenga upya. 
Hii ni kusema kuwa hata taifa ambalo uchumi wake ulikuwa umebomolewa na waovu, sasa roho ya kujenga ndani ya zivu inajenga kwa upya, kupitia wale wote wanaomwabudu MUNGU katika Roho na Kweli.

Mwezi wa Tatu – Siwani- Roho ya kupanda juu (Kut.19:1, Esta8:9)
Musa katika mwezi kama huu aliitwa juu mlimani kupokea sheria ya BWANA, ikimaanisha kuwa hata wewe ambaye umekubali kuingia katika ufalme wa MUNGU sasa hivi ni lazima uinuliwe kwenda juu kwa kasi ya kufumba na kufumbua.
Kule nyuma, nafsi na mioyo ya wengi iliinama sana kupitia njaa, ukiwa, utumwa, utupu, na nira za aina mbali mbali zilizokuwa zinatokana na maagano ya ukoo, kabila, lugha, jamaa, nakadhalika. Kila aliyekuwa anajaribu kubadilisha jamii, kuwa bora, alijikuta anashushwa na uzao wa nyoka.
Unabii wa Siwani ambao ni roho inayoinua moyo na nafsi iliyoinama, unapoungana na yeyote, kama alikuwa amezoea kuomba samaki, sasa atatafuta yeye mwenyewe kufundishwa jinsi ya kuvua samaki. Maana anafunguliwa vifungo vyote vya nira za ujinga. Kumbuka hakuna anayesimama mbele yako tena (Yoshua 1:5)

Mwezi wa Nne–Tamuzi–Macho ya Kanisa (2Fal.25:2-7)

Katika mwezi huu, Ezekia alitobolewa macho ikimaanisha kuwa kanisa lisione tena fursa ambazo MUNGU ameweka mbele yake. Kwa mfano, ukisoma katika Zaburi 82:6MUNGU anatuita miungu na wana wa Aliye juu, lakini kanisa lilikuwa halioni heshima hiyo kwa kuwa uzao wa nyoka ulikuwa umelitoboa macho.
Aidha, katika Mwanzo 2:19 tunasoma jinsi ambavyo MUNGU alifinyanga wanyama na ndege na kumpelekea Adamu ili aone ni jinsi gani atakavyowaita. Majina aliyotamka Adamu ndiyo yaliyokubaliwa na MUNGU.
Macho ya kanisa, katika kipindi hiki cha majira na hatma mpya ya kanisa yamerejeshwa na Roho ya Eliya, kama ilivyotabiriwa na YESU katika Mathayo 17: 9-11 na Marko 9:10-11.
MUNGU ni Roho na anayo nafsi, lakini hutumia hekalu la mwana wa MUNGU, ndipo atende kazi juu ya nchi (Ikorintho 3:16). Macho ya kanisa ni ufahamu wa rohoni au wa mambo ya ufalme wa mbinguni, ambao bila kuwa nayo huwezi kujua kilichoko ndani ya moyo wa MUNGU. Hayo macho ya kanisa ndiyo yameliwezesha kanisa kuelewa maana ya I Korintho 2:6-10, ambayo husema kuwa katika kipindi hiki cha majira na hatma mpya ya kanisa, yatakuwepo mambo ambayo:
+ Jicho halijawahi kuona;
+ Sikio halijawahi kusikia; na 
+ Moyo haujawahi kutafakari.

Tunamshukuru MUNGU kwa ajili ya macho ya kanisa yanayoona hadi ndani ya moyo wa MUNGU, yaliyorejeshwa hivi sasa!

Mwezi wa Tano–Abu–safari za Ufunuo (Hes.33:38-)
Kidunia, tulizoea safari za kutembelea marafiki au kwenda kufanya utalii, wakati mwingine hata kutoka kwa ajili ya kumsema mwingine! Kwa upande wa dini na madhehebu, tulizoea safari za umisionari (kujitolea maisha yako kuhubiri habari za dini na madhehebu, hata kama hukutumwa na MUNGU).
Hivi sasa kila aliyeko katika ufalme wa MUNGU, yaanindani ya miaka 1000 ya kutawala na Kristo kila hatua moja anayopiga ni kwa ajili ya safari ya injili. Hii hutokana na haki, amani na furaha kutawala (Warumi 14:17), ikimaanisha ufalme wa MUNGU aliyeumba mbingu na nchi:
Hivi sasa hakuna tena muda wa kukaa kijiweni bali kila tufanyalo ni katika jina la Bwana, kama ilivyoandikwa katika Wakolosai 3:17.

Mwezi wa Sita– Eluli–Kufanya makuu kwa Muda Mfupi (I Nya.27:9, Neh.6:15)

Katika kitabu cha Isaya 40:28, imeandikwa vazi la MUNGU halina kuchoka wala kuzimia moyo. Ukiangalia kipindi ambacho The Pool of Siloam Church imeanza na mahali ilipofika, ni miaka tisa (9) tu. Lakini kanisalinapatikana katika mikoa yote wakati walionza miaka zaidi ya mia moja (100) iliyopita, hawajafanya hivyo. Huo ni upako wa mwezi Eluli wa kufanya mambo makubwa ndani ya muda mfupi, lakini pia kwa gharama ndogo. Hivindivyo ilivyotokea kwa nehemia, tukisoma katika kitabu chake sura ya 6:15. Ukuta mkubwa sana wa kuzunguka jiji lote la Yerusalemu uliokuwa umebomoka, aliujenga kwa muda wa siku 52 tu! 

Hiki ndicho kipindi cha kuyafanya mambo ya kutisha kwa kuwa nguvu za giza zilizokuwa zinazinga maendeleo ya kanisa zimefutwa zote katika jina la YESU

Mwezi wa Saba–Ethanim-Kuwa juu ya Milima na Vilima (1Fal.8:2, Mwa.8:4)
Katika kipindi cha hiyo miaka 6000 ya utumwa wa kanisa, ukizaliwa katika ukoo masikini ilikuwa haiwezekani tena kujikwamua kutokana na miundo mbinu ya kijamii ambayo ilikuwa haiwezi kuvunjwa na elimu ya dunia au ya dini na dhehebu.

Lakini katika miaka hii 1000 ya kutawala na Kristo YESU, haijalishi kama ulizaliwa katika familia ya kimaskini au tajiri. Kinachotakiwa ni kuvunja misingi yote mibaya ya dini, dhehebu, ukoo, kabila, na umaarufu wa dunia inayosema hakuna MUNGU. Kwa kung’ang’ania na kuungana na kazi iliyofanywa na kanisa kwa miaka tisa (2003-2011), na kukamatia njia na mapito ya BWANA kwenye mlima wake; hakika utakuwa juu ya milima na vilima vya magonjwa, umaskini na kila aina ya maonezi.
Baada ya gharika, safina ya Nuhu ilitua juu ya milima ya Ararati ambayo ndiyo ilikuwa mirefu kuliko yote, hivyo ndivyo ilivyo kwako wewe uliyeingia katika ufalme wa MUNGU, lazima uwe juu ya milima na vilima.

Mwezi wa Nane–Buli–Kurejea kwa Bwana (Zek.1:11, 1Fal.6:38)
Kwa kipindi chote cha miaka 6000, walioko kwenye dini na madhehebu, walikuwa kando ya njia kama Bartimayo, aliyeandikwa katika kitabu cha Marko 10:46-52. Ingawa alijua kuwa YESU anaponya na akimrehemu atapona,kama inavyothibitishwa na Zaburi 103:3, bado alikuwa nje au kando ya njia! Alipogundua kuwa YESU ni njia, na ili akuponye ni lazima utoke kando ya njia, aliruka kutoka porini akaingia njiani wakakutana na YESU. Aidha, alivua mavazi machafu aliyokuwa amevaa ndipo YESU, sasa akamponya.
Katika kipindi hiki cha miaka 6000 ya kutawala na YESU Kristo, tumetoka kando ya njia na tumeingia mahali YESU alipo.Unabii wa Buli ni kuhakikisha kuwa Wana wa MUNGU hawajikwai katika habari ya hekima ya MUNGU katika siri, kama inavyoandikwa katika IKorintho 2:6-10.
Yule ambaye atafikiri kuwa alikuwa na dini na dhehebu nzuri na asifuatane na majira hii, amepotea hakika.

Mwezi wa Tisa – Kisleu-Kutofautishwa (Ezra 10:9, Neh.1:1)
Katika kipindi cha majira iliyopita, ulikuwa huwezi kutofautisha mavazi ya aliyeokoka na ambaye hajaokoka. Aidha, lugha ya aliyeokoka na ambaye hajaokokoka, ilifanana. Wote walilia na kuomboleza (ingawa mmoja kuna kipindi alikuwa anadai anaye MUNGU aliye hai wa kumpigania). 
Sivyo ilivyo katika kipindi hiki cha miaka 1000 ya kutawala na Kristo YESU. Ukiokoka, umeokoka kweli. Katika Isaya 65:13-16 imeandikwa kuwa wakati dunia inalia wewe uliyeokoka unacheka; wakati dunia ina njaa wewe uliyeokoka unakula; wakati dunia ina kiu wewe uliyeokoka unakunywa; wakati dunia na walimwengu wanakimbia majina yao maarufu ambayo yanageuka kuwa laana wewe uliyeokoka unapewa na MUNGU jina la sifa. Huko ndiko kutofautishwa ambako kunafanywa, sasa na unabii au roho ya kutofautishwa ndani ya kisleu.

Mwezi wa Kumi – Thebeti – Kibali cha BWANA (Esta 2:16, Mwa.8:5)
Katika kipindi cha miaka 6000 iliyopita, ukitembea njiani na kitabu cha neno la MUNGU, wengi walikuwa wakikuona wanatema mate chini kuonyesha kuwa wamekutana na mshamba asiyeelewa maisha ya kisasa! Aidha, ulikuwa unatengwa na jamii, maana ilionekana utafilisika! Katika taifa la Uganda, watu wa aina hiyo waliwaita abalokole (neno ambalo lilitoholewa na Kiswahili na kujulikana kama walokole). Hii ina maana ya watu wasio na nyuma wala mbele!


Hivi sivyo ilivyo katika kipindi hiki cha miaka 1000 ya kutawala na Kristo; aliyeokoka, yaani aliyevuliwa mavazi machafu, katika Zakaria 3:3-7 imeandikwa kuwa, atakuwa miongoni mwa wale wasimamao karibu na MUNGU wa majeshi. Hii ina maana ya kibali kwa kila ufanyalo, mpenyo  katika kila jambo. Yale maisha ya kilio, maombolezo kupanda mlima bila kufika kileleni hayapo tena, katika jina la YESU. Msomaji anayesoma haya, akiwa amezungukwa na matatizo anaweza asielewe lakini ndivyo ilivyo maana MUNGU si mtu aseme uongo (Hesabu 23:18-19).
Mwezi wa kumi na Moja – Shebati-Ushindi kila Eneo (Kumb.1:3, Zak.1:7)
Katika mwezi kama huu Musa aliwashinda wafalme wawili wa kipepo walioitwa Ogu na Sihoni ambao walikuwa wakizuia Israeli kwenda mbele.  Halikadhalika kanisa nalo hivi sasa limeshinda wafalme wa kipepo ambao walikuwa wanazuia lisiende mbele, kwa kipindi chote cha miaka 6000 iliyopita.

Inawezekana msomaji ana maumivu, ugonjwa,mafarafano, kukataliwa, moyo unauma na dhiki na adha za aina mbalimbali; kwa majira hii yenye unabii na roho ya kushinda ndani ya shebati, hayo na yote yanayofanana na hayo yameishia katika miaka 6000- hayawezi kuvuka 28 Adari 2011.

Mwezi wa Kumi na Mbili – Adari- Ukuu na enzi (Esta 3:7, Ezra 6:15)
Katika majira ya giza yaliyotawaliwa na wezi na wanyang’anyi (Yoh.10:8), kanisa lilikuwa likianzisha kitu kizuri na Wamidiani wanang’oa (Waamuzi 6:1-10). Maana aliyekuwa anatawala ni ibilisi nyoka wa zamani, kama alivyojitapa katika Mathayo 4:8-9 na Marko 4:5-10.

YESU alipozaliwa katika Luka 1:26-30 tunaona akija na unabii wa ukuu, enzi, kumiliki nyumba ya Yakobo, na kuanza na kumaliza (Alpha na Omega). Unabii huu, kulingana na kitabu cha Efeso 1:22-23 ni wa kanisa, kwa kuwa yeye ni kichwa na kanisa nalo ni mwili wake.

Katika miaka iliyopita, haikuwa rahisi kwa hayo yanayoandikwa hapo juu (aliyokuja nayo YESU) kupokelewa na wahusika, ambao ni kanisa maana mmiliki na mtawala wa uumbaji wote alikuwa ni Joka na uzao wake. Lakini kwa sasa tunamshukuru MUNGU kwa kuwa Ibilisi na uzao hawaingii kulisonga kanisa katika majira hiyo ya miaka 1000 ambapo Kristo mwenyewe ndiye Mfalme wa wafalme (IPetro 2:9-10).

HITIMISHO
Hivi sasa, kila iitwapo leo tunatembea njiani, sokoni, shambani, shuleni, ofisini tukiwa na unabii wa kila siku na kila mwezi kama ilivyoonyeshwa hapo juu. Hiyo ndiyo faida ya majira mpya na hatma ya kanisa. Hata ukiwa safarini ndani ya gari, meli, ndege au chombo cho chote, uko na nguzo ya moto na wingu la moto ambavyo ni MUNGU mwenyewe. Ndiyo maana haiwezekani kwa kanisa kuonewa tena, maana mchungaji ni MUNGU mwenyewe kama ilivyoandikwa katika Zaburi 23:1-3.
Kinachotuingiza kwenye majira halisi  ya MUNGU ni kufuta tarehe za 29, 30, 31 katika kila mwezi  wa kalenda ya Gregori, kwa mamlaka ya MUNGU wa Majeshi,  ili kuondoa uovu wote ulioambatana na hizo siku za ziada kwenye miezi kumi na mbili ya mwaka. Kumbuka nyongeza hiyo ya siku hizo tatu, ilikuwa imesababisha mwezi wa kumi na tatu katika mwaka ambao kiukweli haupo!
Mpangilio wa siku katika kila mwezi sasa umebadilika kama inavyoonyesha hapo chini:
KALENDA YA GREGORI – FEBRUARI 2012 -KIDUNIA 
siku
1
siku

28

2
siku
3
siku
4
siku
5
siku
6
siku
7
27
29
Angalia siku zilivyobadilika  kuingia  abibu  2012!
siku
6
siku
7
siku
1
siku
2
siku
3
siku
4
siku
5
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28



Majira na mpangilio wa siku, miezi, mwaka vimebadilika kabisa; hivyo majira mpya ya kanisa kama ilivyokuwa kabla ya kerubi kuumbwa hii hapa:
Abibu 2012
siku
1
siku
2
siku
3
siku
4
siku
5
siku
6
siku
7
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28

Kwa mantiki hiyo, majira na nyakati sahihi za MUNGU ni kama ifuatavyo, kulingana na majuma saba yaliyo nenwa na Danieli katika Dan.7:25(a):
1
2
3
4
5
6
7
28
2
3
4
5
6
7
1
28
3
4
5
6
7
1
2
28
4
5
6
7
1
2
3
28
5
6
7
1
2
3
4
28
6
7
1
2
3
4
5
28
7
1
2
3
4
5
6
28
28
28
28
28
28
28
28
28
Zile majira au siku za tarehe 29, 30, 31 walizoongeza kwenye kalenda ya Gregori, kulipokuwa na maficho waliyokuwa wanakaa uzao wa nyoka yamefutwa kwa jina la MUNGU wa Majeshi. SASA TUIMBE TUMEPONA.